Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza usitishaji vita kwa "ujumla na wa haraka" kati ya India na Pakistani siku ya , Mei 10. Maadui hao wawili wamehusika katika makabiliano makali ya kijeshi tangu siku ya Jumatano, na mashambulizi ya ndege zisizo na rubani na makombora na kurushiana risasi kwenye mpaka wao unaozozaniwa huko Kashmir.